MMH..YANI FULL MITEGO..HUYU DADA WA HIYARI MI SIMUELEWI JAMANI....!NAOMBENI USHAURI...

Ni mdada tunaheshimiana sana na pengine amekuwa kama adopted sister kwa upande wangu, anajua A - Z kuhusu majanga yangu na wadada wa mjini na pengine anatumia muda wa kutosha kunishauri. Sasa hali ni tofauti siku tatu zilizopita consecutively siku ya kwanza kaniomba nimpeleke akaogelee swimming pool bila shida nikampeleka anachojoa vinguo vyake mbele yangu huku akinitaka tuogelee wote huku viungo vyake vyote tete vinamvuta kila aliye lijali!!!!!!! 


tulichelewa kufika kanitaka twende kwake kwanza kufika kaniganda nilale kwake eti anaogopa nikadhani labda ntalala peke yangu stori stori na mimi mpaka mzee nikahisi usingizi kanipeleka chumbani kulala kanipigisha tena stori hadi nikapitiwa na usingizi bila kujua nimeshituka tumekumbatiana ahsubuhi ila nilijikuta na nguo zangu na yeye yuko na nguo zake alizokuwa amevaa kadai naye alipitiwa na usingizi!!!! Kesho yake kila mtu kashika 50 zake jioni kanitafuta tukapita club tukapiga moja baridi moja moto tukaenda kulala kwake maana anaogopa mpaka apate msichana wa kazi, sijajua kwa kuwa nilikunywa sijui alinishawishije tukalala chumbani kwake nimeamka nikajikuta niko na bukuta yeye na shimizi ila nadhani hatuku du!!!!!!!!!
Kesho yake jioni aliponitafuta nilimwambia najisikia vibaya na nalala kwangu mzee si akaibuka home nikajidai naumwa oh!!!! full huduma mara juisi, mara matunda, mara msosi huku kavaa nusu ut.upu mwisho wa siku kadai hawezi lala mbali na mgonjwa tukalala sote! Sasa leo kadai hawezi kulala wala kushinda bila mimi namheshimu sana jamani sijajua namuepukaje hapa? Kama wewe ulikutwa na mambo haya please wewe ulitatuaje? ndugu zangu nisaidieni 

0 Response to "MMH..YANI FULL MITEGO..HUYU DADA WA HIYARI MI SIMUELEWI JAMANI....!NAOMBENI USHAURI..."

Post a Comment

wdcfawqafwef