Mapenzi
ni kitu Fulani tofauti sana kwenye hii dunia na hata nje ya hii sayari.
Mapenzi kwa kiasi kikubwa sana yanasababisha hata mambo mengine kwenye
hii dunia yaende sawa au yaende tofauti hata kama hayahusiani na
mahusiano ya mapenzi.
Vifo vingi hutokana na mapenzi, kuna
magonjwa watu wanaumwa kisa mapenzi, kuna mambo watu wanayafanya si ya
kawaida kisa mapenzi.
Ukiachilia mbali PESA, Mapenzi
huwa yana nafasi kubwa sana kwenye kitu chochote ndani yahii dunia
tunayoishi. Si masikini wala si tajiri, wote kwa pamoja wanahitaji
mapenzi kutoka kwa wanaowapenda ili dunia iweze kwenda sawa kwa upande
wao. Na ndio sababu hata mimi hapa ninaandika kuhusu mapenzi kwa sababu
yananigusa hata mimi na hata wewe unayesoma hapa sasa.
Ukipata mpenzi anayekuelewa na kukupenda basi hata dunia iwe ya tabu
vipi kwako utaiona inazunguka kama kawaida na maisha yatasonga mbele
kwako kwa raha mustarehe, na hata matatizo mengine makubwa kwako huwa
madogo kwa sababu tu unapenda na kupendwa kwa dhati.
Lakini ukiumizwa kwenye mapenzi au kutojaliwa kama wewe unavyojali basi
hata dunia iwe na raha gani kwako utaiona chungu na hata raha ya maisha
hutakuwa nayo hata kama una hela kiasi gani na hata kama una cheo
kikubwa kama mfalme au hata rais. Wengine hufikia hatu ya kuteseka tu
bila kuondoka kwenye mahusiano kwa kuogopa kuumizwa tena huko waendapo
na wengine huondoka baadae sana wakiwa tayari wameshachelewa.
Kuna Sababu Nyingi Sana zinazoweza kusababisha mapenzi kupungua kwenye
mahusiano yenu na wakati mwingine hata kusababisha kuachana. Mojawapo
kati ya sababu hizo ni pamoja na hizi zifuatazo;-
1. UONGO.
Hakuna kitu kibaya kama uongo kwenye mapenzi, uongo wa aina yoyote ile
si mzuri kwa wanaopendana kwa dhati kwa sababu huweza kupunguza mapenzi
na uaminifu kwa kiasi kikubwa sana miongoni mwa wanaopendana hasa kama
mmojawapo akigundua kuwa mwenzi wake ni muongo/anamdanganya.
Kuna vitu vingine hata kudanganyana
haileti maana wala haina tija kwa hiyo kuwa mkweli kwa mpenzi wako kwa
lolote lile ni jambo jema sana kuliko kuwa unamdanganya kila siku hadi
aje kugundua unamdanganya itakuwa matatizo na unaweza kusababisha
kuachana.
2. USIRI WA KUPITILIZA.
Miongoni mwa vitu hatari pia kwenye mahusiano ni pamoja na hili la usiri
wa kupitiliza. Kama una vitu moyoni na upo kwenye mapenzi/mahusiano
bora kabisa si vizuri kuvificha na hasa vile vinavyohusiana na mapenzi
yenu moja kwa moja. Ni kweli kuna vingine huwezi kumwambia kwa sababu
havina mahusiano ya moja kwa moja na mahusiano yenu ila kuna vingine ni
lazima avijue ili kutoleta ugomvi au matatizo hao baadae.
Kama kuna kitu hukuwahi kumwambia na unahisi ukimwambia atakasirika ni
bora umtafutie nafasi nzuri umwambie kuliko aje kugundua mwenyewe
itakuwa shida sana kukuelewa, kwa mfano mpo kwenye mahusiano mwaka wa 4
sasa na kumbe kabla ya kuwa na yeye ulishawahi kuoa/kuolewa na una
watoto 2 kwa huyo mke/mume wa mwanzo ni bora umwambie kuliko kumficha,
anaweza kukuelewa lakini mara nyingi ni kwa shingo upande.
3. ANA-CHEAT/ANA MTU MWINGINE.
Hakuna kitu kinauma kwenye love kama kugundua kuwa Yule unayempenda
tena kwa dhati na kumjali kwa kila kitu halafu yeye kumbe ana mtu
mwingine zaidi ya wewe.
Huwa inauma sana na mara nyingi
huwa inasababisha hata wengine kuweza kuondoka kwenye mahusiano hata
kama walikuwa bado wanapenda pale walipo. Hakuna binadamu anayependa
kuwa ‘’option’’ kwenye mapenzi.
Kamwe Usimuumize Moyo
Akupendaye Kiukweli, Usimfanye Ajutie Penzi Lako, Usimfanye Anung'unike
Kwa Unayomtendea, Unaweza Kuona Ni Ujanja Lakini Ipo Siku Utahitaji
Mapenzi Ya Kweli Kwa Mwingine Na Hutayapata, Laana Ya Mapenzi Ipo,
Ukimuumiza Ipo Siku Nawe Utaumia Tu, Mapenzi Ya Kweli Yanawezekana Kama
Ukiamua na si kwa ku-cheat.
4. DHARAU.
Hii pia huchangia kwa kiasi kikubwa kupunguza mapenzi kama sio
kuyamaliza kabisa. Unapokuwa kwenye uhusiano jitahidi kumpenda mtu wako
kwa khali yoyote na usiwe na dharau kwake au hata kwa marafiki zake au
ndugu zake au hata wengineo. Hakuna mtu anayependa mtu mwenye dharau
hata awe nani.
Na hii huwa mara nyingi inatokea pale
mmojawapo kati ya wanaopendana akimzidi mwenzake uwezo iwe kwa cheo,
pesa,uzuri au hata akili na mara nyingi sana inatokea kwa wasichana
pale wanapokuwa wapo juu ya wapenzi wao kiuwezo, ila wasichana
wanatakiwa kutambua kuwa Linapokuja Suala La Ndoa/Kuishi Na Mtu, Kwetu
Sie Wanaume Huwa Hatuangalii Uzuri/Urembo Wa Mwanamke Kama Ndio Kigezo
Pekee Cha Kufanya Tumuoe/Tuishi Na Huyo Mwanamke, Ingekuwa Hivyo Basi
Wanawake Wote Warembo/Wazuri Wangekuwa Ndani Ya Ndoa Leo Hii, Hii
Inamaanisha Kuwa Hata Ukiwa Mrembo/Mzuri Hutakiwi Kujisahau Ukaona
Umeshafika...Utapotea ukileta dharau kwa uzuri wako au uwezo ulionao.
5. MROPOKAJI/ASIYE MSIRI.
Hakuna kitu kinachoweza kumfanya mwenza wako kukukimbia au hata kukosa
uaminifu na wewe kama akija kugundua kama wewe ni mropokaji na huna
‘’kifua’’ hasa kwa yale mambo ambayo ni ya chumbani na hayakutakiwa
kutoka nje. Hakuna mtu anayependa siri zake kutoka hadharani na huwa
inaumiza sana kwenye mapenzi kumpa mtu siri zako then yeye anaenda
kusimulia.
Mambo mnayafanya mkiwa wawili tena ndani lakini
kesho unaenda mtaani unakuta kila mtu anajua mlichofanya tena
wanakuhadithia kama walikuwepo vile, hiyo si kitu nzuri na itakufanya
ukimbiwe na kila mpenzi unayempata.
6. TAMAA/KUKOSA UVUMILIVU.
Tamaa ni kitu kingine ambacho hufanya mahusiano mengi kukosa nguvu na
mengine kuvurugika kabisa. Kama mpo kwenye mapenzi na mmeamua kupendana
kwa shida na raha basi haitakiwi mmoja wenu kuwa na tama na kukosa
uvumilivu hata kwa yale mambo yanayoweza kuzuilika.
Kama
mpenzi wako ni wa hali Fulani na umeamua kuwa naye basi usiwe na tama
kwa vitu vingine ambavyo vinaweza kukusababishia mahusiano yako kukosa
nguvu na kufa kabisa. Amini kuwa ipo siku mtakuwa na vitu kama
unavyotamani kwa kuongeza bidii kutafuta na kushauriana nini cha kufanya
lakini si kwa kutafuta ‘’shotcut’’/njia nyepesi nyepesi zinazoweza
kuku-cost hapo baadae.
7. KUKOSA MSIMAMO.
Hii kitu huwakuta wengi sana kwenye mapenzi ya siku hizi. Nadhani ni
hali halisi ya dunia ya sasa inachangia pia pamoja na teknolojia
tuliyonayo ya kutuwezesha kufanya yale tunayoyaona kwenye mitandao na
vyombo mbali mbali vya habari.
Wapenzi wengi siku hizi
wamekosa msimamo kwenye mapenzi/mahusiano yao na unakuta tu mmoja
anakuwa na wapenzi zaidi ya mmoja na wanakuwa hawafahamiani huku kila
mmoja akijua kuwa yeye ndo kila kitu kwa mpenzi wake.
8. KUTOJALI/KUTOKUWA NA MSAADA.
Hii pia kwa kiasi kikubwa inaumiza sana na kupelekea kushuka kwa
thamani ya mapenzi miongoni mwa mahusiano mengi haa duniani. Kama kweli
unampenda mpenzi wako basi msaidie anapopata matatizo na umjali na
kumchukulia kama mpenzi wako na mtu wako wa karibu na sio kukimbia
majukumu bila sababu zote za msingi.
Kama huwezi kujali na kusaidia basi usiingie kwenye mahusiano ni bora ukae mwenyewe kuliko kuwepo sehemu usiyotakiwa.
9. UBAHILI.
Huna sababu yoyote ya kuwa na pesa na mpenzi wako akawa anapata tabu
kama vile humuoni. Sijasema utoe pesa hata kwa mambo yasiyo na msingi
lakini at least utimize majukumu yako kwa mpenzi wako kila
unapohitajika.
Kuna vitu vingine hata huhitaji
kuambiwa kama unatakiwa kuvishughulikia, ni wewe mwenyewe tu kuwa
responsible kumhudumia mpenzi wako. Na hii huwa ina-apply sana kwa
wavulana kutokana na kasumba iliyojengeka na mila tulizozikuta.
10. USHOGA/USAGAJI
Hii ipo wazi kabisaaaaaaa…. Hakuna mtu anayependa mtu wake awe Shoga
kama ni mvulana au awe Msagaji kama ni msichana. Ni aibu kubwa sana kwa
mpenzi wako kuwa katika makundi haya mawili na sidhani kwa akili ya
kawaida kama unaweza kufurahia hiki kitu kama utakisikia au kama
utakishuhudia kwa
Tuesday 11 March 2014
0 Response to "EPUKA HIZI SABABU 10 ZINAZOWEZA KUSABABISHA NDOA AMA MAPENZI KUVUNJIKA."
Post a Comment